ZOEZI LA CHANJO YA HIARI KWA WAFANYAKAZI
Katika kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya sita chini ya uongozi makini wa Rais Mh. Mama Samia Suluhu Hassan, Tanzania Commercial Bank kwa kushirikiana na Hospitali ya Kairuki Mikocheni tumefanya zoezi la chanjo ya hiari kwa Wafanyakazi wa benki, ndugu, jamaa, marafiki na jirani zake walio katika maeneo ya karibu ya makao makuu ya benki yaliyopo jengo la PSSSF Tower II gorofa ya 10 eneo la Makumbusho jijini Dar Es Salaam.
Kwenye picha ni Mkurugenzi wa Rasilimali watu na utawala wa benki Bi. Diana Myonga na Dr. Erick Heri kutoka Hospitali ya Kairuki Mikocheni wakiongea na waandishi wa habari kabla ya kuanza zoezi hilo.