MKUTANO WA WANAHISA WA BENKI 2021
Tanzania Commercial Bank imefanya mkutano na wanahisa na kujivunia kwa kupata faida kabla ya kodi ya Shilingi bilioni 21 kwa mwaka 2020. Akizungumza kwenye mkutano huo Menyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki Dkt. Edmund Mndolwa alisema benki inaendelea kufanya vizuri licha ya changamoto mbalimbali zilizojitokeza kwa mwaka jana hasa jana la Corona na imeahidi kufanya vizuri zaidi kwa mwaka 2021 na kuboresha huduma zinazotolewa na benki.