LAUNCH OF PARTNERSHIP WITH AIRTEL
Tanzania Commercial Bank na Airtel wameungana pamoja kupata suluhisho la huduma za fedha kidigitali nchini. Taasisi hizi mbili zimeingia ubia kwa lengo la kuboresha na kupanua wigo wa huduma za kifedha nchini kupitia huduma za Airtel Money, itasaidia Mawakala wa Airtel Money ambao wataweza kununua float kwenye tawi lolote la TPB na wateja wote wa Airtel Money wataweza kufanya miamala yote kupitia Tanzania Commercial Bank.
Kwenye picha ni Mkurugenzi wa Uendeshaji na Tehama wa benki, Bw. Jema Msuya na Mkurugenzi wa Airtel Money Bw. Isack Nchunda wakizindua rasmi huduma hiyo. Wengine kwenye picha ni Menejimenti ya Tanzania Commercial Bank.